Maafisa wa polisi kutoka gatundu kaskazini kwa wiki ya pili sasa wanatafuta magenge ya vijana ambao wamekuwa wakiiba mifugo na kuuza nyama hizo katika maeneo ya gatunyu na mangu kaunti ya kiambu. Wenyeji wamepoteza zaidi ya mifugo ishirini katika visa ambavyo wanasema vimekuwa vikiendelea bila ya wao kupata usaidizi wowote kutoka kwa maafisa wa usalama. Mwanahabari wetu gatete njoroge ametuandalia taarifa hiyo